.
Samatta kaanza mechi za play offs Ubelgiji kwa kufunga katika ushindi wa 4-0

Ligi Kuu Ubelgiji imeendelea tena jana Jumamosi ya April 1 2017 kwa KRC Genkinayochezewa na mtanzania Mbwana Samatta kuikaribisha Lokeren katika mchezo wao wa kwanza wa play offs wa Kundi B wa Ligi Kuu Ubelgiji.
Mbwana Samatta ambaye alikuwa katika kikosi cha kwanza cha KRC Genk kilichocheza dhidi ya Lokeren alifanikiwa kuisaidia timu yake ya KRC Genk kupata ushindi wa goli 4-0,Mbwana Samatta akifunga goli la pili dakika ya 72.

Goli la kwanza la Genk lilifungwa na Pozuelo dakika ya 45, goli la tatu lilifungwa na Boetiusdakika ya 77 la mwisho lilifungwa na Jose Naranjo aliyeingia dakika ya 84 akitokea benchi na kufunga goli dakika ya 90, ushindi huo umeifanya KRC Genk kuongoza Kundi B lenye timu sita kwa kuwa na magoli mengi.
Taarifa kuhusu stori za nyasi bandia za Simba kupigwa mnada na TRA

Lakini kuna taarifa pia zilizotolewa baadae kuwa mtanzania Mbwana Samatta aliyewahi kucheza Simba ambaye kwa sasa anaichezea KRC Genk ya Ubelgiji amezilipia kodi hizo, ukweli kutoka katika ukurasa rasmi wa msemaji wa Simba Haji Manara na TRA ni kuwa Samatta hajalipia kodi ya nyasi hizo.

Ukweli wa taarifa rasmi ni kuwa Simba wameongezewa muda wa siku 14 wazilipie kodi nyasi zao hizo bandia ambazo wanampango wa kuziweka katika uwanja wao wa mazoezi wa Bunju, katika siku 14 walizopewa Simba tayari zimebakia siku tatu pekee
MATOKEO YA STARS NA BURUNDI LEO
Taifa stars imewaadhibu BURUNDI Kwa jumla ya magoli 2 - 1
magoli ya stars yakiwekwa kambani na Simon Msuva pamoja na Mbaraka Yusufu wakati goli pekee la burundi likiwekwa kambani na mchezaji wa klabu ya Simba sc Laudit Mavugo. Mpaka dakika ya mwisho Stars 2 na BURUNDI 1.
magoli ya stars yakiwekwa kambani na Simon Msuva pamoja na Mbaraka Yusufu wakati goli pekee la burundi likiwekwa kambani na mchezaji wa klabu ya Simba sc Laudit Mavugo. Mpaka dakika ya mwisho Stars 2 na BURUNDI 1.
STARS vs AMAVUBI (BURUNDI) LEO JIONI NDANI YA AZAM TV ...MAVUGO NDANI
Taifa Stars ya Tanzania leo Machi 28, 2017 saa 10:00 jioni
inaingia tena Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, kucheza na Intamba
Murugamba ya Burundi katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa, kwa mujibu
wa kalenda ya wiki ya mechi za kimataifa ya FIFA.
Huu ni mchezo wa pili kwa Taifa Stars kucheza ndani ya wiki moja
baada ya ule wa awali dhidi ya The Zebras ‘Pundamilia’ wa Botswana
uliofanyika Uwanja huo wa Taifa, jijini Dar es Salaam Jumamosi
iliyopita.
Katika mchezo huo wa Jumamosi, Taifa Stars ambayo kwa sasa inanolewa
na Salum Mayanga akisaidiwa na Patrick Mwangata ambao ni makocha wapya
wa kikosi hicho, walishinda kwa mabao 2-0.
Tayari Intamba Murugamba wametua nchini tangu juzi Jumapili saa 4.30
asubuhi na kufikia Hoteli ya De Mag iliyoko, Kinondoni, Dar es Salaam na
jioni yake walifanya mazoezi kwenye Uwanja wa Karume, Ilala jijini. jana
Jumatatu, inafanya mazoezi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Ndani ya kikosi hicho wamo washambuliaji wawili wanaotamba katika
klabu za Simba na Young African za Dar es Salaam. Nyota hao ni Amisi
Tambwe wa Young Africans na Laudit Mavugo wa Simba.
Jana Jumatatu Machi 27, 2017 saa 8.30 alasiri nyota hao wakiongozana
na kocha wao watazungumza na wanahabari namna walivyoajiandaa kucheza na
Taifa Stars ambayo pia ina nyota wengi wanaocheza na wachezaji hao wa
Burundi katika klabu za Simba na Young Africans.
Wakati Mavugo ni mshambuluaji, anatarajiwa kuwa na wakati mgumu mbele
ya walinzi mahiri ambao pia wako Simba kama vile Abdi Banda na Mohammed
Hussein wakati Andrew Vicent anayetoka Young African atakuwa kisiki kwa
Tambwe wanayecheza naye timu moja kama makocha watawapanga.
Kwa upande wake, Mayanga alifurahishwa na ushindi wa Jumamosi
iliyopita dhidi ya The Zebras ya Botswana na hivyo amehimiza Watanzania
kujitokeza kwa wingi katika mchezo wa kesho.
Katika kuunga mkono wito wa Kocha Mayanga, TFF imebakiza viingilio
vya mchezo huo kuwa sawa na vile vya Jumamosi iliyopita kwani katika
mzunguko ambao unachukua mashabiki wengi kiingilio kitakuwa ni Sh 3,000.
Kwa upande wa VIP “A” Kiingilio kitakuwa ni Sh 15,000 wakati VIP “B”
na VIP “C” kiingilio kitakuwa ni Sh 10,000. Viingilio hivyo vimelenga
kuwaalika Watanzania wengine kwenda uwanjani.
Subscribe to:
Posts (Atom)


































